Elizabeth Michael (Lulu)
...........
BreakingNews : Msanii Maarufu Lulu Michael anayekabiliwa na tuhuma za mauaji ya Msanii mwenzake Steven Kanumba amepata dhamana leo.Ambapo alitakiwa kuwa na wadhamini wawili na Sh20m kila mmoja.
Masharti aliyopangiwa ambayo ni
pamoja na kuwasilisha hati yake ya kusafiria, kutosafiri nje ya Dar es
salaam, kujiwakilisha au kuripoti mahakamani kila siku ya kwanza ya kila
mwezi pamoja na wadhamini wake wawili ambao kila mmoja adhamini kwa
shilingi milioni 20 za kitanzania.
Upande wa familia ya Lulu
umesema masharti yote yaliyotajwa wanaweza kuyatimiza leo leo hivyo
wanasubiri tu jibu la msajili ambae ndio anatakiwa kuhakikisha hayo
masharti yametimia kisha ruhusa ya kumkabidhi Lulu kwa familia yake
itolewe.
Wiki iliyopita mawakili wa muigizaji huyo waliwasilisha maombi ya dhamana kwa mahakama hiyo kuu ya Tanzania.
Wanasheria hao Peter Kibatala, Kennedy Fungamtama na Fulgence Massawe waliomba dhamana hiyo itolewe haraka kwakuwa muombaji amekaa mahabusu kwa zaidi ya miezi saba na kwamba kosa lake linaweza kupewa dhamana.
Lulu anakabiliwa na kesi ya kumuua bila kukusudia Steven Kanumba April 7, 2012, huko Sinza Vatican, jijini Dar es Salaam.
Kanumba alidaiwa kuwa kwenye ugomvi na Lulu aliyekuwa mpenzi wake nyumbani kwake Sinza.
SOURCE: ITV
Wanasheria hao Peter Kibatala, Kennedy Fungamtama na Fulgence Massawe waliomba dhamana hiyo itolewe haraka kwakuwa muombaji amekaa mahabusu kwa zaidi ya miezi saba na kwamba kosa lake linaweza kupewa dhamana.
Lulu anakabiliwa na kesi ya kumuua bila kukusudia Steven Kanumba April 7, 2012, huko Sinza Vatican, jijini Dar es Salaam.
Kanumba alidaiwa kuwa kwenye ugomvi na Lulu aliyekuwa mpenzi wake nyumbani kwake Sinza.
SOURCE: ITV
Post a Comment